Jeremiah 6:11-12


11 aLakini nimejaa ghadhabu ya Bwana,
nami siwezi kuizuia.

“Wamwagie watoto walioko barabarani,
na juu ya vijana waume waliokusanyika;
mume na mke watakumbwa pamoja ndani yake,
hata nao wazee waliolemewa na miaka.

12 bNyumba zao zitapewa watu wengine,
pamoja na mashamba yao na wake zao,
nitakapounyoosha mkono wangu
dhidi ya wale waishio katika nchi,”
asema Bwana.
Copyright information for SwhKC